KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, March 24, 2013

KALA JEREMIAH AJA NA KARIBU DAR ES SALAAM


MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Kala Jeremiah ameibuka na kibao kipya kinachokwenda kwa jina la Karibu Dar es Salaam.

Akizungumza na Burudani mjini Dar es Salaam juzi, Kala alisema tayari kibao hicho kimeshaanza kupigwa kwenye vituo vya redio na kuonyeshwa kwenye vituo mbalimbali vya televisheni nchini.

Kala, ambaye ni mmoja wa wasanii walioibuliwa kupitia shindano la Bongo Star Search (BSS) alisema, kibao hicho kinaelezea matatizo ya maisha yanayowakumba vijana katika jiji la Dar es Salaam.

Katika kibao hicho, Kala anasimulia jinsi watu wenye maisha ya juu wasivyojua shida ya maji, chakula na usafiri wakati wale wenye maisha ya dhiki, maji kwao ni sawa na almasi.

Kala amerekodi kibao hicho huku kibao chake cha Dear God kikiwa bado kinaendelea kutamba kwenye vituo vya redio na luninga.

Msanii huyo alisema kwa sasa hana mpango wa kurekodi albamu mpya kwa vile bado albamu yake ya Pasaka inaendelea kufanya vizuri sokoni.

"Utaratibu wangu kwa sasa ni kurekodi wimbo mmoja mmoja, sina mpango wa kurekodi albamu. Kama ni kutafuta pesa, nitategemea zaidi matamasha ya muziki,"alisema msanii huyo.

No comments:

Post a Comment