KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 14, 2013

2FACE: NITAMTOSHELEZA MKE WANGU KIMAPENZI



LAGOS, Nigeria
MWANAMUZIKI nyota wa Nigeria, 2Face Idibia ameahidi kumtosheleza mkewe, Annie Macaulay masuala yote yanayohusu unyumba.

2Face alitoa ahadi hiyo wakati wa ndoa ya kimila iliyofungwa mwishoni mwa wiki iliyopita katika viwanja vya shule ya Apostolic vilivyopo Urua.

Ndoa hiyo ilifungwa mbele ya baadhi ya wanasiasa maarufu wa Nigeria, Godwill Akpabio (Gavana wa Jimbo la Akwa) na Florence Ita Giwa.

Wakati wa ndoa hiyo, 2Face aliulizwa maswali mbalimbali, ikiwa ni pamoja na iwapo ataweza kumtosheleza mkewe kitandani.

Huku akicheka na kuonyesha kulifurahia swali hilo, 2Face alijibu kwa kusema, ataweza kumtosheleza mkewe bila matatizo yoyote. Jibu hiyo lilisababisha kicheko kutoka kwa watu waliohudhuria sherehe hiyo.

Wakati huo huo, Gavana Akpabio ameamua kumzawadia 2Face Idibia na mkewe Annie Macaulay, gari jipya aina ya Prado SUV.

Gavana Akpabio alitoa zawadi hiyo wakati wa ndoa ya 2Face na Annie iliyofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mwanasiasa huyo pia aliahidi kupeleka ujumbe wa watu 30 mjini Dubai kwa ajili ya sherehe ya wanandoa hao inayotarajiwa kufanyika baadaye mwezi huu.

No comments:

Post a Comment