KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 14, 2013

SIPENDI KUWA CHEMBEMBE-INI EDO



LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu machachari wa Nigeria, Ini Edo ameamua kuwapa ujumbe mashabiki wa fani hiyo wanaompenda na kumchukua.

Ini ameamua kutoa ujumbe huo, kufuatia shutuma nyingi zilizoelekezwa kwake kuhusu kuongezeka uzito kwa kiwango kikubwa.

Katika ujumbe huo, alioutoa kupitia akaunti yake ya twitter, Ini amesema kamwe hapendi kuwa mwembamba.

Mcheza filamu huyo, ambaye ni mzaliwa wa Jimbo la Akwa aliandika hivi: "Asanteni wapenzi wangu kwa kunipa moyo. Kwa wale wanaonichukia, kamwe sipendi kuwa mwembamba. Siku zote nitaendelea kuwa mwanamke wa kiafrika."

Mashabiki wanaomshutumu Ini kwa kuongezeka uzito wanadai kuwa, amepoteza uzuri na urembo wake.

Ini alifunga ndoa mwishoni mwa mwaka jana na Philip Ehiagwina, anayeishi na kufanyakazi nchini Marekani, ambaye amekuwa akimuelezea kuwa ni shujaa wake na kipenzi chake.

No comments:

Post a Comment