KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 14, 2013

SEMINA ELEKEZI COPA COCA-COLA MACHI 19



SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limesema, semina elekezi kwa ajili ya michuano ya Copa Coca-Cola 2013, inatarajiwa kufanyika Machi 19 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, washiriki wa semina hiyo wanatakiwa kuripoti kwenye ofisi za shirikisho hilo Machi 18 mwaka huu.

Alisema washiriki hao ni makatibu wa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa ya Tanzania Bara na Zanzibar.

Aliwataja washiriki wengine kuwa ni waratibu wa mikoa wa mashindano ya Umoja wa Michezo wa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA).

Wambura alisema barua za mwaliko kwa ajili ya semina hiyo tayari zimetumwa kwa vyama vya mpira wa miguu vya mikoa.

No comments:

Post a Comment