KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 14, 2013

WALIOIUA CAMEROON WAITWA TENA TAIFA STARS

KOCHA Mkuu wa timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars, Kim Poulsen ametangaza majina ya wachezaji 23 watakaoingia kambini Jumamosi kwa ajili ya kujiandaa kwa mechi dhidi ya Morocco.

Mechi hiyo ya michuano ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia za 2014 zitakazofanyika Brazil, itachezwa Machi 24 mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa Kim, wachezaji hao wanatakiwa kuripoti kambini Machi 15 mwaka huu katika hoteli ya Tansoma iliyopo barabara ya Nyerere, Dar es Salaam.

Wachezaji walioitwa ni makipa Juma Kaseja kutoka Simba ambaye pia ndiye nahodha, Aishi Manula (Azam), Hussein Shariff (Mtibwa Sugar) na Mwadini Ally (Azam).

Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Erasto Nyoni (Azam), Issa Rashid (Mtibwa Sugar), Kelvin Yondani (Yanga), Nadir Haroub (Yanga), Nassoro Masoud Cholo (Simba) na Shomari Kapombe (Simba).

Viungo ni Salum Abubakar (Azam), Athuman Idd (Yanga), Amri Kiemba (Simba), Khamis Mcha (Azam), Frank Domayo (Yanga), Mwinyi Kazimoto (Simba) na Shabani Nditi (Mtibwa Sugar).

Washambuliaji ni John Bocco (Azam), Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu (TP Mazembe,Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo- DRC), Mrisho Ngasa (Simba) na Simon Msuva (Yanga).

Benchi la ufundi la Taifa Stars linaundwa na Sylvester Marsh (kocha msaidizi), Juma Pondamali (kocha wa makipa), Leopold Tasso (meneja), Dk. Mwanandi Mwankemwa (daktari wa timu), Frank Mhonda (mtaalamu wa tibamaungo) na Alfred Chimela (mtunza vifaa).

No comments:

Post a Comment