KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 14, 2013

KIVAZI CHA GENEVIEVE CHAZUA GUMZO



LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu nyota wa Nigeria, Genevieve Nnaji mwishoni mwa wiki iliyopita alikuwa kivutio kikubwa wakati wa sherehe za utoaji wa tuzo za AMVCA zilizofanyika mjini hapa.

Sababu iliyomfanya Genevieve awe kivutio kwa watu waliohudhuria sherehe hiyo ni kivazi alichokuwa amevaa, ambacho kiliacha sehemu kubwa ya kifua chake kikiwa wazi.

Gauni hilo jeupe alilovaa mwanadada huyo lilisababisha sehemu ndogo ya matiti yake yote mawili kuonekana na hivyo kuwatoa udenda akina yakhe.

Baadhi ya mapaparazi waliohudhuria sherehe hiyo walipigana vikumbo, kila mmoja akitaka kupata picha nzuri za mcheza filamu huyo, ambaye muda wote huo alionekana akitabasamu.

Maziwa madogo ya mwanadada huyo na chuchu zilizosimama mithili ya msichana aliyevunja ungo, ndivyo vitu vilivyokuwa kivutio kutoka kwa mwanadada huyo.

Mbali na hayo, sura yake mwanana na umbile lenye mvuto ni baadhi ya vitu vingine vilivyomfanya awe kivutio cha aina yake wakati wa sherehe hiyo.

Baadhi ya mapaparazi walijaribu kumuuliza maswali mcheza filamu hiyo, lakini hakufunua mdomo wake kujibu chochote.

Hata hivyo, baada ya muda, Genevieve aliamua kubadili kivazi hicho na kuvaa kivazi kingine kirefu cha rangi nyekundu, iliyomeremeta ambacho kilimfanya azidi kupendeza.

No comments:

Post a Comment