KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, October 31, 2012

YANGA WANACHEEKA, SIMBA WAMENUNA


Mchezaji Simon Msuva (kushoto) wa Yanga akikabwa koo na beki wa Mgambo JKT wakati wa mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara iliyochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Yanga imeshinda mabao 3-0. (Picha kwa hisani ya BIN ZUBEIRY).

YANGA jana ilionyesha dhamira yake ya kuwapoka uongozi wa ligi kuu ya Tanzania Bara wapinzani wao wa jadi Simba baada ya kuicharaza Mgambo JKT mabao 3-0 katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Ushindi huo uliiwezesha Yanga kuwa na pointi sawa na Simba, lakini inazidiwa kwa tofauti ya mabao ya kufunga na kufungwa na watani wao hao, ambao leo wamelazimishwa sare ya bao 1-1 na vibonde, Polisi Morogoro.
Mabao ya Yanga yalipachikwa wavuni na beki Nadir Haroub 'Cannavaro, Didier Kavumbagu na Jerry Tegete.
Nayo Simba ilijikuta majaribuni baada ya Polisi Morogoro kuwa ya kwanza kupata bao kupitia kwaa mshambuliaji wake, Mokili Rambo.
Simba ilisawazisha kipindi cha pili kwa bao lililofungwa na kiungo wake mahiri, Amri Kiemba.

No comments:

Post a Comment