KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, October 30, 2012

POULSEN AMALIZA ZIARA ZENJI



Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania, Kim Poulsen amerejea Dar es salaam baada ya kufanya ziara kwenye visiwa vya Pemba na Unguja ambako alishuhudia mechi sita za Ligi Kuu ya Grand Malta kuanzia Oktoba 19, 2012 hadi Oktoba 26, 2012 visiwani Zanzibar. Poulsen alishuhudia mechi baina ya Falcom na Bandari iliyoisha kwa Falcom kushinda kwa mabao 3-1 na pia mechi baina ya Duma na Bandari ambayo iliisha kwa Bandari kuibuka na ushindi wa mabao 2-0. Mechi hizo mbili zilifanyika kisiwani Pemba.

Poulsen pia alishuhudia mechi zilizofanyika kwenye Uwanja wa Amaan kisiwani Unguja ambako Mtendeni iliibwaga Chipukizi kwa mabao 2-1; Mundu na Jamhuri (0-1), KMKM na Zimani Moto (1-0); na Mafunzo dhidi ya Chuoni iliyoisha kwa Mafunzo kulala kwa mabao 3-0.
Poulsen amefurahishwa na ziara hiyo na kusema kuwa ni kitu kizuri kwake na kwa soka la Tanzania kwa ujumla. Poulsen alisema kuwa amefurahishwa na mapokezi aliyopata visiwani Zanzibar na kukishukuru Chama cha Mpira wa Miguu cha Zanzibar (ZFA) kwa ushirikiano mkubwa alioupata wakati wote akiwa Zanzibar.
Hata hivyo, Poulsen alisema hawezi kueleza kwa sasa kama ameona wachezaji anaoweza kuwaita kwenye kikosi cha Taifa Stars, lakini akasema amevutiwa na viwango vya wachezaji wengi.

No comments:

Post a Comment