KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, October 23, 2012

SIMBA, MGAMBO JKT ZAINGIZA MIL 33/-



MCHEZO baina ya Simba Sports Club ya Jijini Dar es salaam na Mgambo Shooting uliofanyika katika uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga umeingiza mapato ya jumla ya sh 33,303,000 kupitia viingilio vya watazamaji 5260 walioushuhudia mechi hiyo.
Meneja wa Uwanja wa Mkwakwani,Mbwana Msumari alitoa taarifa hiyo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mapato yaliyopatikana katika mchezo huo ambao matokeo yalikuwa sare ya kutofungana.
Alitoa mchanganuo kwa kusema kuwa, idadi ya watazamaji walioingia na kukaa katika jukwaa kuu ni 811 waliokata tiketi za sh 10,000 kwa kila mmoja zikakusanywa sh 8,110,000 huku jukwaa lijulikanalo kwa jina la Old Tanga ambalo ni maarufu kwa kukaliwa na mashabiki wa timu ya Coastal Union walikaa watazamaji 1474 waliolipa kiingilio cha sh. 7,000 kila mmoja na kupatikana sh 10,314,000.
Msumari alisema idadi ya watazamaji walioingia uwanjani hapo na kukaa Jukwaa maarufu kwa jina la Russia ilifikia 2975 waliolipa kiingilio cha sh 5,000 kwa kila mmoja zikapatikana jumla ya sh 14,875,000.
Alisema kupitia mapato hayo Simba na Mgambo Shooting kila moja ilipata kiasi cha sh 7,002,409.50 na shirikisho la soka nchini TFF liliweka kibindoni sh 1,068,164.16 huku mmiliki wa uwanja wa Mkwakwani ambaye ni chama cha Mapinduzi CCM ikipewa sh 3,560,547.20.
Kwa mapato hayo,Meneja huyo alisema imeonyesha kwamba timu ya Mgambo Shooting imekubalika na kufanikiwa kupata wapenzi wengi kutoka eneo lote la Mkoa wa Tanga.

No comments:

Post a Comment