KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, October 30, 2012

UCHAGUZI DRFA DESEMBA 12



TFF imebadilisha tarehe ya kuanza kuchukua fomu kwa watu wanaotaka kugombea uongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu cha Dar es salaam (DRFA) kwa lengo la kuhakikisha kuwa mchakato wa uchaguzi unafanyika kwa mujibu wa kanuni. Kamati ya Uchaguzi ya DRFA ilitangaza jana kuwa uchukuaji fomu ungeanza leo, lakini DRFA iliandikiwa barua jana kuelezwa kuwa mchakato huo sasa utaanza kesho na uchaguzi utafanyika Desemba 12, 2012.
Mchakato wa uchaguzi wa viongozi wa DRFA utakuwa kama ifuatavyo:
30/10/2012 Kamati ya Uchaguzi DRFA kutangaza uchaguzi na nafasi
zinazogombewa kwa mujibu wa katiba ya DRFA
31/10/2012 Kuanza kuchukua fomu za kugombea uongozi
04/11/2012 Mwisho wa kurudisha fomu ifikapo saa 10:00 alasiri
05-09/11/2012 Kamati ya Uchaguzi DRFA kupitia fomu za waombaji uongozi na kutangaza matokeo na kubandika kwenye mbao majina ya waombaji uongozi.
10-14/11/2012 Kutoa fursa ya pingamizi dhidi ya waombaji uongozi. Pingamizi ziwasilishwe kwa katibu wa Kamati ya Uchaguzi DRFA na
wawekaji pingamizi wazingatie Ibara ya 11 (2) ya Kanuni za
Uchaguzi za Wanachama wa TFF.
15-17/11/2012 Kujadili pingamizi, usaili na kutangaza matokeo ya usaili na
kuwajulisha kwa maandishi.
18-20/11/2012 Kukataa rufaa dhidi ya maamuzi ya Kamati ya Uchaguzi ya DRFA
21-25/11/2012 Rufaa kusikilizwa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF na kutangaza matokeo ya rufaa (Kama hakuna rufaa, Kamati ya Uchaguzi ya
DRFA kutangaza majina ya wagombea na nafasi wanazogombea
na kuanza kampeni).
26/11/2012 Baada ya maamuzi ya Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Kamati ya
Uchaguzi ya DRFA kutangaza majina ya wagombea na nafasi zao na kuanza kwa kampeni
12/12/2012 Uchaguzi

No comments:

Post a Comment