KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, October 24, 2012

COSSY AFANYA VITUKO SIKU YAKE YA KUZALIWA



LAGOS, Nigeria
MWANADADA Cossy Orjiakor mwishoni mwa wiki iliyopita alifanya kioja cha mwaka baada ya kuwakaribisha wageni aliowaalika kwenye hafla ya siku yake ya kuzaliwa kwa kucheza muziki kwa staili ya aina yake.
Mcheza filamu huyo, ambaye pia ni mwimbaji na mcheza shoo, aliandaa sherehe hiyo nyumbani kwake, nje kidogo ya mji wa Lagos na kuwaalika rafiki zake mbali mbali.
Wakati wageni hao walipoanza kuwasili nyumbani kwake, mwanadada huyo aliyekuwa amevaa nusu uchi, alikuwa akiwakaribisha kwa kucheza dansi kwa staili ya kumwaga lazi.
Baadhi ya wageni hao walionekana kufurahishwa na staili hiyo ya Cossy na kumtaka arudie kucheza mara kwa mara, lakini wengine walione aibu.
Hafla hiyo ilihudhuriwa na wacheza filamu wachache pamoja na waandishi wa habari wa vyombo mbali mbali.
Cossy si mwigizaji maarufu sana nchini Nigeria, lakini ni machachari kutokana na kuandamwa na kashfa mbali mbali kwenye vyombo vya habari.
Mwaka jana, Cossy aliamua kutengana na mpenzi wake baada ya kushindwa kumnunulia gari aina ya Range Rover Sport Jeep wakati wa sherehe yake ya kuzaliwa.
Baada ya kutengana na mpenzi wake huyo, Cossy aliamua kujitosa kimapenzi kwa mwanasoka, Abumere Ededuan.
Baadhi ya mashuhuda wameueleza mtandao wa nigeriafilms kwamba, Cossy na Abumere, ambaye kwa sasa ni wakala wa wachezaji, anayetambuliwa na Shirikisho la Soka la Dunia (FIFA), wamekuwa wakionekana sehemu mbali mbali za starehe pamoja.
Mashuhuda hao wamesema, mapenzi ya Cossy na mchezaji huyo wa zamani wa Nigeria, ni mwanana mithili ya watu waliojitosa kwa mara ya kwanza katika ulimwengu huo.

No comments:

Post a Comment