KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, October 30, 2012

AZAM YAMTIMUA BUNJAK, YAMREJESHA STEWART


KLABU ya Azam imetangaza kumtimua kocha wake, Boris Bunjak kutoka Serbia na kumrejesha kocha wa zamani, John Stewart Hall.
Uamuzi huo wa bodi ya wakurugenzi ya Azam, umekuja siku chache baada ya timu hiyo kuchapwa mabao 3-1 na Simba katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara iliyochezwa kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Taarifa iliyotolewa na Azam leo imesema kuwa, Bunjak ameondolewa kutokana na kushuka kwa kiwango cha timu hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Stewart anatarajiwa kurejea nchini Alhamisi kutoka Kenya, ambako alikuwa akiifundisha timu ya Sofapaka.

No comments:

Post a Comment