KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, October 21, 2012

SIMBA KUNANI? YATOKA SARE TENA NA MGAMBO JKT

MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya Tanzania Bara, Simba leo wameendelea kuchemsha baada ya kulazimishwa kutoka suluhu na Mgambo JKT katika mechi iliyochezwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.
Licha ya kulazimishwa sare, Simba bado inaendelea kuongoza ligi hiyo kwa kuwa na pointi 19 baada ya kucheza mechi tisa, lakini inaweza kuenguliwa kileleni na Azam, iwapo itashinda mechi yake dhidi ya Ruvu Shooting Jumatano ijayo kwenye uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.
Katika mechi nyingine ya ligi hiyo iliyochezwa leo, JKT Ruvu ilitoka sare ya bao 1-1 na ndugu zao wa JKT Oljoro katika mechi iliyochezwa kwenye uwanja wa Chamazi wakati Prisons iliichapa Toto African bao 1-0 kwenye Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.

No comments:

Post a Comment