KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Tuesday, October 30, 2012

NSA JOB NJE KWA WIKI SITA




MSHAMBULIAJI nyota wa Coastal Union, Nsa  Job atakuwa nje ya uwanja kwa wiki sita kufuatia kuvunjika mguu wake wa kushoto.
Nsa alipatwa na maswaibu hayo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati Coastal Union ilipomenyana na JKT Ruvu katika mechi ya ligi kuu ya Tanzania Bara iliyochezwa kwenye uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.
Kwa sasa, mshambuliaji huyo amefungwa plasta ngumu na atakosa mechi zote zilizosalia za raundi ya kwanza ya ligi hiyo.
Mkurugenzi wa Ufundi wa Coastal Union, Nassor Bin Slum amesema goti la mshambuliaji huyo liligeuka, lakini madaktari wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili walifanikiwa kulirejesha kwenye sehemu yake.
Kwa mujibu wa Bin Slum, mchezaji huyo anatarajiwa kupelekwa India kwa ajili ya matibabu zaidi ya mguu wake ili aweze kuendelea kucheza soka.

No comments:

Post a Comment