KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, August 29, 2013

USAILI WAGOMBEA TFF, BODI KUANZA KESHO



Usaili kwa wanaoomba kuteuliwa kuwa wagombea uongozi katika uchaguzi wa
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na ule wa Bodi wa Ligi Kuu (TPL Board)
unaanza kesho (Agosti 30 mwaka huu).

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Kamati ya Uchaguzi ya TFF, Agosti 30 mwaka
huu ni usaili kwa waombaji uongozi wote katika Bodi ya Ligi Kuu pamoja na waombaji
uongozi wa TFF kwa kanda namba 11 (Morogoro na Pwani), kanda namba 12
(Kilimanjaro na Tanga) na kanda namba 13 (Dar es Salaam).

Agosti 31 mwaka huu ni kanda namba sita (Rukwa na Katavi), kanda namba saba
(Mbeya na Iringa), kanda namba nane (Njombe na Ruvuma), kanda namba tisa
(Lindi na Mtwara) na kanda namba kumi (Dodoma na Singida).

Usaili kwa kanda namba moja (Geita na Kagera), kanda namba mbili (Mara na
Mwanza), kanda namba tatu (Simiyu na Shinyanga), kanda namba nne (Arusha na
Manyara) kanda namba tano (Kigoma na Tabora), na nafasi za Rais na Makamu
wa Rais wa TFF utafanyika Septemba Mosi mwaka huu.

Waombaji wote wamepangiwa muda wao wa usaili. Kwa mujibu wa ratiba usaili
ufanyika kuanzia saa 3 kamili asubuhi hadi saa 2 usiku. Wasailiwa wote wanatakiwa
kuzingatia muda waliopangiwa.

Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

No comments:

Post a Comment