KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Saturday, August 10, 2013

SIMBA KUTAMBULISHA NYOTA WAKE WAPYA LEO, INACHEZA NA SC VILLA YA UGANDA




TIMU ya soka ya Simba leo itatambulisha nyota wake wapya wakati itakapocheza mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya SC Villa ya Uganda.

Mechi hiyo itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ni sehemu ya maadhimisho ya tamasha la Simba Day, ambalo hufanyika kila mwaka kabla ya kuanza kwa ligi kuu.

Katibu Mkuu wa Simba, Evod Mtawala alisema jana kuwa, wachezaji watakaotambulishwa leo ni pamoja na mshambuliaji wa kimataifa wa Burundi, Hamisi Tambwe na beki wa kimataifa wa nchi hiyo, Kaze Gilbert.

Wachezaji wengine wapya watakaotambulishwa leo ni beki Joseph Owino na mshambuliaji, Betram Mombeki.

Mtawala alisema mechi hiyo itapambwa na burudani kutoka kwa wasanii wa muziki wa kizazi kipya wa kundi la TMK Wanaume Family na Snura, anayetamba kwa kibao chake kipya cha Majanga.

Wakati huo huo, Coastal Union ya Tanga leo itawatambulisha nyota wake wapya wakati itakapocheza mechi ya kirafiki dhidi ya kombaini ya Polisi.

Mkurugenzi wa Ufundi wa Coastal Union, Nassor Bin Slum alisema jana kuwa,mechi hiyo itapigwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.

Aliwataja wachezaji wapya watakaotambulishwa leo kuwa ni Haruna Moshi 'Boban', Juma Nyoso, Yayo Lutimbi kutoka URA ya Uganda na Crispin Odula kutoka Bandari ya Kenya.

No comments:

Post a Comment