KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, August 29, 2013

COPA COCACOLA KANDA KUANZA SEPT 2



Michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15
inayoshirikisha mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani inaanza kutimua vumbi
Septemba 2 mwaka huu katika vituo sita tofauti.

Kwa mujibu wa ratiba iliyopangwa leo (Agosti 29 mwaka huu), kituo cha Mwanza
mechi zake zitachezwa katika viwanja vya Alliance ambapo timu zitakazofungua
dimba ni Kagera vs Kigoma, Mara vs Tabora, Simiyu vs Geita na Mwanza vs
Shinyanga.

Kituo cha Mbeya ambapo mechi zitachezwa viwanja vya Iyunga ni Katavi vs
Njombe, na Ruvuma vs Mbeya. Kituo cha Pwani ni Ilala vs Kaskazini Unguja, na
Lindi vs Pwani.

Ufunguzi katika kituo cha Arusha ambapo mechi zake zitachezwa Uwanja wa
Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta AMri Abeid ni Manyara vs Kilimanjaro, na Arusha vs
Singida.

Uwanja wa Jamhuri ambapo utatumika kwa mechi za kituo cha Morogoro, Tanga
itacheza na Dodoma wakati Morogoro itaumana na Temeke. Mjini Zanibar kwenye
Uwanja wa Chuo cha Amaan ni kati ya Kaskazini Pemba na Mjini Magharibi, na Kusini
Pemba dhidi ya Kusini Unguja.

No comments:

Post a Comment