KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 23, 2012

Papic ataka mazoezi usiku


KOCHA Mkuu wa Yanga, Kostadin Papic ameutaka uongozi wa klabu hiyo kuiandalia timu mazoezi ya usiku kwa ajili ya kujiandaa kwa mechi ya marudiano dhidi ya Zamalek ya Misri.
Papic anataka Yanga ifanye mazoezi usiku kwa vile mechi yao ya marudiano dhidi ya Zamalek itachezwa katika muda huo.
Kiongozi mmoja wa Yanga alisema jana kuwa, watalifanyia kazi ombi hilo la Papic kwa vile ni la muhimu ili wachezaji waweze kuizoea hali hiyo.
“Ni kweli Papic amewasilisha ombi hilo kwa uongozi na tumeshaanza kulifanyia kazi. Kwa vile mechi yetu ya marudiano itachezwa usiku, ni vizuri wachezaji waizoee hali hiyo mapema,”alisema.
Yanga na Zamalek zinatarajiwa kurudiana wiki mbili zijazo mjini Cairo na upo uwezekano mechi hiyo ikachezwa bila watazamaji ama ikahamishiwa katika nchi nyingine.
Katika mechi ya awali iliyochezwa mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1.
Kutokana na sare hiyo, kila timu inayo nafasi ya kusonga mbele iwapo itashinda mechi ya marudiano. Hata hivyo, Zamalek itakuwa na faida kubwa ya kucheza ugenini.

No comments:

Post a Comment