KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 23, 2012

TFF yafuta uchaguzi wa DRFA


KAMATI ya Uchaguzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imetangaza kufuuta uchaguzi mkuu wa Chama cha Soka mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) ulioapangwa kufanyika Machi 18 mwaka huu.
Taarifa iliyotolewa na mwenyekiti wa kamati hiyo, Deogratias Lyatto kwa vyombo vya habari jana ilisema kuwa, uchaguzi huo umefutwa kutokana na katiba ya DRFA kutokidhi matakwa ya katiba ya TFF.
Kwa mujibu wa Lyatto, mchakato wa uchaguzi wa DRFA sasa utaanza upya mara baada ya kukamilika kwa marekebisho ya vifungu vya katiba ya chama hicho vinavyokinzana na matakwa ya katiba ya TFF kabla ya Agosti 10 mwaka huu.
Kufuatia uamuzi huo, kamati hiyo imesema uongozi wa sasa wa DRFA utaendelea kukaa madarakani hadi uchaguzi huo utakapofanyika kabla ya Agosti mwaka huu.
Lyattu alisema kamati yake imefikia uamuzi huo kwa kuzingatia ushauri wa kamati ya sheria, katiba na hadhi kwa wachezaji kuhusu katiba ya DRFA.
“Kamati iliridhika na kukubaliana na ushauri wa kamati ya sheria, katiba na hadhi kwa wachezaji kwamba, katiba ya DRFA haikidhi matakwa ya katiba ya TFF,”alisema.

No comments:

Post a Comment