KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, February 22, 2012

Mwisho, Meryl wapata mtoto wa kike


MWAKILISHI wa Tanzania katika shindano la Big Brother Africa mwaka 2008, Mwisho Mwampamba na mpenzi wake, Meryl wa Namibia wamepata mtoto.
Habari za kuaminika kutoka kwenye mitandao mbalimbali zimeeleza kuwa, Meryl amejifungua mtoto wa kike mwishoni mwa wiki iliyopita mjini Whindhoek.
Mwisho na Meryl walishiriki katika shindano hilo mwaka 2008, ambapo Mwisho alishika nafasi ya pili nyuma ya Makubale wa Zambia, aliyeibuka mshindi.
Mwisho na Meryl walifunga ndoa mwaka 2011 baada ya kuonyeshana mapenzi mazito wakati wa shindano la Big Brother Africa-All Stars lililowashirikisha nyota wa zamani.
Kujifungua kwa Meryl ni mwendelezo wa baadhi ya washiriki wa shindano hilo kufunga ndoa na kupata watoto. Mwaka jana, washiriki wengine wa shindano hilo, Kevin wa Nigeria na Elizabeth Gupta wa Tanzania walipata mtoto wa kike.
Katika mwendelezo huo, pia wamo Quinn Sieber wa Afrika Kusini na Jennifer wa Msumbiji, ambao wanatarajia kupata mtoto hivi karibuni.
Kabla ya kushiriki shindano la Bib Brother Africa-All Stars, Mwisho alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki nyota wa kizazi kipya nchini, Rehema Chalamila ‘Ray C’, lakini haukudumu kwa muda mrefu.
Mtanzania huyo pia amejitokeza kuwa mwigizaji bora wa filamu, ambapo mbali na kucheza filamu kadhaa za kibongo, pia amewahi kucheza filamu mbili za Kinigeria.

No comments:

Post a Comment