KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 16, 2012

Davina aibukia filamu ya Diana


BAADA ya ukimya wa muda mrefu, hatimaye msanii chipukizi wa filamu nchini, Halima Yahaya ‘Davina’ amerejea kwenye fani hiyo kwa kishindo.
Safari hii, Davina amecheza filamu mpya, inayojulikana kwa jina la Diana, ambayo imeongozwa na gwiji wa fani hiyo, Single Mtambalike ’Richie’.
Kuibuka upya kwa Davina kumekuja miezi kadhaa baada ya kudaiwa kuwa, aliamua kuipa fani hiyo kisogo kutokana na masuala ya uzazi.
Davina alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, kwa sasa yupo tayari kwa ajili ya kazi na kuonyesha maajabu.
“Baada ya mapumziko ya muda, narudi kwa nguvu, nakuja na filamu ya Diana,”alisema mwanadada huyo mwenye sura na umbo lenye mvuto.
”Ni filamu ambayo kila mtazamaji atakapoitazama, ataikubali. Unajua uwezo bado ninao, lakini kutokana na majukumu, niliamua kupumzika kidogo na sasa ni kazi tu,”alisema mwanadada huyo.
Kwa upande wake, Richie alisema baadhi ya wasanii huamua kupumzika kutokana na kutingwa na majukumu mengine ya kimaisha na si kumalizika kiusanii.
”Davina ni msanii mwenye kipaji na bado ana uwezo mkubwa katika fani na hilo litathibitika ndani ya filamu ya Diana,”alisema.
Mbali na Davina, wasanii wengine walioshiriki kucheza filamu hiyo ni Juma Chikoka ’Chopa’ na Catherine.

No comments:

Post a Comment