KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, February 22, 2012

Chelsea hoi kwa Napoli


NAPLES, Italia
MABAO yaliyofungwa na Ezequiel Lavezzi na Edinson Cavan jana yaliiwezesha Napoli ya Italia kuibwaga Chelsea ya England katika mechi ya awali ya mtoano ya ligi ya mabingwa wa Afrika iliyochezwa mjini hapa.
Katika mechi hiyo, Napoli iliichapa Chelsea mabao 3-1 na kujiweka kwenye nafasi nzuri ya kufuzu kucheza hatua ya robo fainali.
Kipigo hicho kimeziweka timu za England kwenye nafasi finyu ya kufuzu kucheza robo fainali, kufuatia wiki iliyopita Arsenal kupigwa mweleka wa mabao 4-0 na AC Milan ya Italia.
Katika mechi hiyo iliyokuwa na ushindani mkali, Chelsea ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 27 kupitia kwa mshambuliaji wake, Juan Mata kufuatia uzembe wa nahodha wa Napoli, Paolo Cannavaro.
Levezzi aliisawazishia Napoli dakika ya 38 baada ya kupokea pasi akiwa ndani ya mita 18 na kufumua shuti kali lililomshinda kipa Petr Cech wa Chelsea. Mabao hay
Cavani aliiongezea Napoli bao la pili baada ya kumtoka beki mmoja wa Chelsea kabla ya kumtengenezea pasi murua Levezzi aliyeongeza bao la tatu dakika ya 65. Licha ya kupata kipigo hicho, Kocha Mkuu wa Chelsea, Andre Villas-Boas alijigamba kuwa, bado wanayo matumaini ya kushinda mechi ya marudiano na kusonga mbele.
“Tuna hakika tunaweza kubadili matokeo kwenye uwanja wa Stamford Bridge kwa sababu ya nafasi tulizopata usiku wa leo. Napoli walikuwa makini mbele ya goli lakini sisi hatukuweza kufanya hivyo. Tulifanya makosa mengi na Napoli walitumia nafasi hiyo,”alisema.
Kocha huyo alikiri pia kuwa, atalazimika kuifanyia marekebisho safu yake ya ulinzi kwa vile ilichangia kwa kiasi kikubwa wapinzani wao kupata mabao mawili ya kwanza.
Katika mechi hiyo, Chelsea ilicheza bila ya nahodha wake, John Terry, ambaye ni majeruhi na anatarajiwa kufanyiwa operesheni hivi karibuni itakayomfanya akae nje ya uwanja kwa wiki sita.
Kocha Mkuu wa Napoli, Walter Mazzarri alisema timu yake ilikuwa na uwezo wa kushinda mabao manne, ambayo yangeiweka kwenye nafasi nzuri katika mechi ya marudiano itakayochezwa mjini London.
“Chelsea ilicheza vizuri kama tulivyotarajia,lakini tuliwazidi mbinu, hasa katika ushambuliaji. Tulikuwa na wakati mgumu dakika 15 za kwanza, lakini baada ya kusawazisha, tulitulia na kucheza vizuri,”alisema.
Hata hivyo, Walter alikiri kuwa pambano lao la marudiano litakuwa gumu kwa vile wapinzani wao wanao uwezo wa kupata mabao mawili nyumbani.

No comments:

Post a Comment