KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 9, 2012

Zambia kucheza fainali na Ivory Coast

Wachezaji wa Zambia wakipongezana baada ya timu hiyo kuifunga Ghana bao 1-0 jana

Wachezaji wa Ivory Coast wakimpongeza mchezaji mwenzao, Gervinho baada ya kuifungia bao pekee dhidi ya Mali jana.

LIBREVILLE, Gabon
IVORY Coast na Zambia jana zilifuzu kucheza fainali ya michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika baada ya kuibuka na ushindi dhidi ya Mali na Ghana.
Katika mechi hizo zilizokuwa na ushindani mkali, Ivory Coast iliichapa Mali bao 1-0 wakati Zambia nayo iliipiga Ghana mweleka wa idadi hiyo ya bao.
Bao pekee la Ivory Coast lilifungwa na mshambuliaji Gervinho katika kipindi cha kwanza, kufuatia uzembe wa mabeki wa Mali.
Katika mechi hiyo, Ivory Coast ilitawala vipindi vyote viwili huku washambuliaji wake, Didier Drogba na Yaya Toure walikosa nafasi kadhaa za kufunga mabao.
Nayo Zambia ilijipatia bao lake la pekee dakika ya 78 kupitia kwa mshambuliaji wake, Emmanuel Mayuka, aliyetokea benki.
Hii ni mara ya kwanza kwa Zambia kufuzu kucheza fainali ya michuano hiyo katika kipindi cha miaka 18 iliyopita na sasa itakutana na Ivory Coast katika mechi ya kutafuta bingwa, itakayochezwa Jumapili.
Ghana ilifanikiwa kupata penalti dakika ya nane iliyopigwa na Asamoah Gyan, lakini iliokolewa na kipa Kennedy Mweene wa Zambia.
Waghana walilazimika kumaliza mechi hiyo wakiwa na wachezaji 10 baada ya Derek Boateng kutolewa nje kwa kadi nyekundu dakika za mwisho.

No comments:

Post a Comment