KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, February 22, 2012

Nina usongo na muziki- Rich Mavoko


MSANII anayechipukia katika muziki wa kizazi kipya nchini, Rich Mavoko amejigamba kuwa, ana hasira na usongo wa muziki.
Rich ametoa majigambo hayo wiki hii wakati ambapo kibao chake kipya cha Silali kimekuwa kikitamba katika vituo mbalimbali vya radio na televisheni nchini.
Alisema anamshukuru Mungu kuona kwamba, kibao chake hicho kimepokelewa vizuri na mashabiki na kinashika namba moja kwenye chati mbalimbali za radio.
“Wimbo mmoja, lakini mafanikio kibao. Hii ni ishara njema kwamba huko mbele mambo yatakuwa mazuri zaidi,”alisema.
Rich alisema licha ya ugeni wake katika fani, yeye ni msanii aliyekamilika kwa vile ana uwezo mkubwa wa kuimba na kurapu.
Alisema kimuziki, ameamua kufuata nyayo za msanii Diamond, ambaye amemuelezea kuwa ana kipaji cha hali ya juu kimuziki.
“Nampenda sana Diamond kwa sababu yupo kivyake vyake na anakubalika kote,”alisema.
Rich alisema kwake, anamuona Diamond kama msanii aliyekaa kizaramo zaidi kutokana na aina ya muziki anaopiga na ujumbe wake kwa jamii.

No comments:

Post a Comment