KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, February 12, 2012

BURIANI WHITNEY HOUSTON!






MWANAMUZIKI nyota wa Marekani na mcheza filamu nguli wa Holywood, Whitney Houston amefariki dunia ndani ya chumba cha hoteli ya Beverly Hilton mjini Los Angeles.

Mwili wa Houston (48) ulikutwa bafuni ndani ya chumba alichopanga na kuna habari kuwa, kabla ya kifo chake, alitumia dawa za kulevya na pombe. Mwanamuziki huyo alifariki saa 9.55 alasiri.

Hadi sasa, chanzo cha kifo cha mwanamuziki huyo hakijafahamika japokuwa Ijumaa jioni, alikuwa na baadhi ya rafiki zake wakinywa pombe katika baa ya hoteli hiyo.

Whitney alipangwa kutumbuiza katika sherehe za utoaji wa tuzo za Grammy, lakini mauti yalimkumba saa chache kabla ya sherehe hizo kuanza.

Gari la polisi liliwasili katika hoteli hiyo dakika chache baada ya muhudumu kupiga simu akieleza kwamba kuna mtu amekufa kwenye moja ya vyumba vilivyomo ghorofa ya nne.

Whitney alikuwa gwiji wa muziki wa pop na ndiye mwanamuziki anayetajwa kwamba, alikuwa na sauti nzuri. Baadhi ya nyimbo zake zilizompatia umaarufu mkubwa ni pamoja na I will always love you na Saving all my love for you.

Whitney alianza kujihusisha na utumiaji wa dawa za kulevya baada ya kufunga ndoa na mwanamuziki mwingine nyota wa nchi hiyo, Bob Brown, aliyezaa naye mtoto mmoja wa kike, Bobbi Kristina.

Polisi wa Los Angeles wamesema inaweza kuchukua wiki sita hadi nane kuweza kubaini chanzo cha kifo cha mwanamuziki huyo.

No comments:

Post a Comment