KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, February 22, 2012

DUDU BAYA: Nani kasema nimefilisika?


BAADA ya ukimya wa muda mrefu, msanii nyota wa zamani wa muziki wa kizazi kipya, Godfrey Tumaini ameibuka na kusema si kweli kwamba ukimya wake kimuziki umetokana na kuishiwa.
Tumaini, ambaye ni maarufu zaidi kwa jina la Dudu Baya alisema mjini Dar es Salaam wiki hii kuwa, ukimya wake umetokana na kujihusisha kwake zaidi na mambo ya biashara.
Alisema amefikia uamuzi wa kufanya biashara kwa vile hapendi kutegemea muziki katika maisha yake yote.
Alisema kupitia kampuni yake ya promosheni ya Tumaini Entertainment na ile ya ujenzi ya Mambaz Timbers, amekuwa akifanya vitu tofauti kwa lengo la kujiendeleza kimaisha.
Dudu Baya alisema yeye ni msanii tofauti na wengine wa muziki wa kizazi kipya nchini kwa sababu hategemei sana muziki huo kuendesha maisha yake.
“Sio kweli kwamba nimefilisika. Nimeamua kuiga maisha ya wasanii wengine walioendelea kimuziki kama vile Robert Kelly,”alisema.
“Nimekuwa nikiitumia kampuni yangu ya Tumaini Entertainment kuandaa maonyesho na matamasha mbalimbali ya muziki. Nachukua bendi na wasanii, nawaandalia maonyesho,”aliongeza.
Dudu Baya alisema kampuni yake ya Mambaz Timbers inajihusisha na utengenezaji na uuzaji wa vifaa vya ujenzi na kwamba, anamshukuru Mungu mambo yake yanakwenda vizuri.

No comments:

Post a Comment