KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, February 8, 2012

Ndoa ya Aki yajibu mapigo




LAGOS, Nigeria
NDOA ya mcheza filamu nyota wa Nigeria, Chinedu Ikedieze na mkewe, Nneoma imejibu mapigo baada ya kuelezwa kuwa, tayari mwanadada huyo amepata uja uzito.
Chinedu, maarufu kwa jina la Aki, alifunga ndoa na Nneoma mwishoni mwa mwaka jana na kuhudhuriwa na watu mbalimbali maarufu nchini Nigeria, akiwemo Rais wa nchi hiyo, Goodluck Jonathan.
Mmoja wa watu walio karibu na Aki ameueleza mtandao wa Nigeriafilms kuwa, kwa sasa mwili wa Nneoma umeongezeka uzito na ameanza kunenepa katika kila sehemu ya mwili wake.
Alipoulizwa iwapo taarifa hizo ni za kweli, Aki aling’aka na kuvitaka vyombo vya habari viache kufuatilia maisha yake na mkewe.
“Mimba? Hapana! Mnapaswa kutuacha kama tulivyo. Tunapaswa kuweka mambo yetu sawa kwanza kabla ya kuzaa watoto,”alisema Aki.
“Tafadhali tuacheni tufurahie maisha yetu ya ndoa,”aliongeza msanii huyo, aliyeanza kujipatia umaarufu mkubwa kupitia filamu ya Aki na Ukwa, aliyoicheza kwa kushirikiana na swahiba wake mkubwa, Osita Iheme ‘Ukwa’.
Siku chache baada ya kufunga ndoa, Aki alikaririwa akisema kuwa, yeye na mkewe wangependa kuwa na watoto wawili au watatu bila kujali jinsia yao.
Aki na mkewe walirejea nchini Nigeria mwishoni mwa mwezi uliopita, wakitokea Abu Dhabi, Muungano wa Falme za Kiarabu (UAE) walikokwenda kwa mapumziko.
Wanandoa hao walikaa Abu Dhabi kwa siku saba kwa ajili ya mapumziko maalumu ‘honeymoon’ na wanatarajia kuondoka tena Nigeria wiki ijayo kwenda Marekani.
Kwa mujibu wa mtandao wa Nigeriafilms, Aki na mkewe wamepanga kwenda Marekani kwa ajili ya sherehe ya siku ya wapendanao (Valentine Day).
Akizungumza na mtandao huo, Aki aliyaelezea mapumziko yao huko Abu Dhabi kuwa yalikuwa ya aina yake na kwamba walipata nafasi ya kutembelea sehemu mbalimbali zenye vivutio vya kitalii.
Inakadiriwa kuwa, Aki alitumia Naira milioni tano za Nigeria kwa ajili ya matembezi hayo, ambapo walipanga kwenye hoteli ya nyota nne ya Sheraton.

No comments:

Post a Comment