KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, February 8, 2012

Bakhresa ajitosa kutetea kiti chake DRFA


WAGOMBEA watatu zaidi wamejitokeza kuchukua fomu za kuwania uenyekiti katika uchaguzi wa Chama cha Soka mkoa wa Dar es Salaam (DRFA).
Miongoni mwa wagombea hao ni pamoja na Amin Bakhresa, ambaye anatetea nafasi hiyo. Wagombea wengine ni Salum Mkemi na Salum Mwaking'anda.
Mratibu wa Kamati ya Uchaguzi ya DRFA, Harudiki Kabunju alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, uchukuaji wa fomu ulitarajiwa kuhitimishwa saa 10 jioni.
Alimtaja mgombea mwingine aliyejitokeza kuchukua fomu jana kuwa ni Benny Kisaka, anayewania nafasi ya kuziwakilisha klabu katika mkutano mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Uchaguzi mkuu wa DRFA, ambao umekuwa ukisubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka nchini, umepangwa kufanyika Machi 18 mwaka huu.
Akizungumza uamuzi wake kutetea nafasi ya uenyekiti, Bakhresa alisema umetokana na malengo aliyojiwekea ya kukuza na kuendeleza soka katika mkoa wa Dar es Salaam.
Bakhresa alisema changamoto bado ni nyingi na ili atimize malengo yake, ameona ni vyema aendelee kukiongeza chama hicho.
Wagombea wengine waliochukua fomu ni Gungulungu Tambaza na Khamisi Kisiwa (makamu mwenyekiti), Selemani Salim Kigodi (ujumbe wa kamati ya utendaji),Ramadhani Kampira na Mohammed Bhinda (ujumbe wa klabu) na Ally Hassan (mweka hazina).
Wengine, nafasi wanazowania zikiwa kwenye mabano ni Muhsin Balhabou (ujumbe wa TFF), Kanuti Daudi (ujumbe wa kamati ya utendaji), Msanifu Kondo (katibu mkuu), Abeid Mziba, Hamisi Mkwama (ujumbe) na Lameck Nyambaya (ujumbe wa klabu).

No comments:

Post a Comment