KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, February 16, 2012

GENEVIEVE: Nimechoka kuishi pweke, nataka kuolewa


LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu nyota wa Nollywood, Genevieve Nnaji amekiri kuwa, amechoka kuishi mpweke na sasa anataka kuolewa na kuwa na familia.
Genevieve amesema ameishi pweke kwa miaka mingi na kwamba anajisikia vibaya pale anapowaona rafiki zake wengi wakiwa wameolewa.
Mcheza filamu huyo anayeshika namba tano kwa utajiri miongoni mwa waigizaji wa kike wa Nollywood, alisema hayo wiki hii kupitia mtandao wa twitter.
Kauli hiyo ya Genevieve ilitokana na mmoja wa rafiki zake wa utotoni, kumtumia picha ya siku ya harusi yake kupitia blackberry.
“Nimechoka kuishi maisha ya upweke, rafiki zangu wengi sasa wameolewa,”alisema Genevieve akimweleza rafiki yake huyo.
Kwa kipindi kirefu sasa, Genevieve amekuwa akihusishwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki nyota wanchi hiyo, D’Banj, lakini wote wawili wamekuwa wakikanusha madai hayo.
Genevieve na D’Banj walikaririwa kwa nyakati tofauti wakisema kuwa, uhusiano wao ni wa kawaida, kama vile wa kaka na dada.
Wakati huo huo, baadhi ya ndugu na marafiki wa mwigizaji mwingine nyota wa nchi hiyo, Rita Dominic wamemtaka aachane na maisha ya usichana, badala yake afunge ndoa.
Rita, ambaye anashika nafasi ya tatu kwa utajiri miongoni mwa waigizaji wa kike wa Nollywood, amekuwa akihusishwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mcheza filamu mwenzake, Jim Iyke.
Hata hivyo, urafiki wao ulikufa baada ya Jim kuonekana kuwa hayupo tayari kufunga ndoa na Rita.
Ndugu na marafiki hao wamemweleza Rita kuwa, muda wa kuishi kiusichana umekwisha na kwamba kwa sasa anahitaji kuwa na mume na watoto.
Rita pia amekuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanaume kadhaa, lakini hakuna yeyote kati yao aliyeonyesha dhamira ya kutaka kumuoa.

No comments:

Post a Comment