KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Sunday, February 12, 2012

Zambia mabingwa Afrika














LIBREVILLE, Gabon
TIMU ya soka ya taifa ya Zambia, Chipolopolo juzi iliweka historia ya aina yake baada ya kutwaa ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika kwa kuibwaga Ivory Coast kwa penalti 8-7 katika mechi kali na ya kusisimua ya fainali iliyochezwa mjini hapa.
Mshindi wa pambano hilo ilibidi apatikane kwa njia ya penalti tano tano baada ya timu hizo kumaliza dakika 120 zikiwa suluhu.
Katika kupigiana penalti tano tano, wachezaji nyota wa Ivory Coast, Didier Drogba, Yaya Toure na Gervinho walipoteza.
Zambia imetwaa kombe hilo miaka 19 tangu wanasoka na viongozi wake 18 walipofariki katika ajali ya ndege iliyotokea mwaka 1993 nchini Gabon. Zambia ilirejea Gabon kwa lengo la kuweka historia ya kuwaenzi wanasoka hao.
Drogba ndiye aliyeikosesha Ivory Coast ushindi baada ya kupoteza penalti yake ndani ya dakika 90 baada ya shuti lake kupaa juu ya lango.
Zambia: Mweene,Musonda (Nyambe Mulenga 11), Sunzu, Himonde, Nkausu, Sinkala, Lungu, Chansa, Christopher Katongo, Kalaba, Mayuka, Nyambe Mulenga (Felix Katongo 74).
Subs Not Used: Kalililo, Kasonde, Mbesuma, Chamanga, Chivuta, Chintu, Kangwa, Sakuwaha, Titima.
Booked: Nyambe Mulenga.
Ivory Coast: Barry, Tiene, Toure, Bamba, Gosso, Zokora (Konan 75), Tiote, Toure Yaya (Bony 86), Gervinho, Kalou (Gradel 63), Drogba.
Subs Not Used: Yeboah, Boka, Doumbia, Coulibaly, Keita, Lolo, Eboue,Gnanahouan.Booked: Tiote, Bamba.
Referee: Badara Diatta (Senegal).

No comments:

Post a Comment