KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, October 27, 2011

YANGA: Tutamlipa Timbe haki zake zote



KLABU ya Yanga imesema inatarajia kumalizana na kocha wake wa zamani, Sam Timbe kabla ya mechi yao dhidi ya Simba keshokutwa.
Mjumbe wa kamati ya utendaji ya Yanga, Mohamed Bhinda alisema mjini Dar es Salaam jana kuwa, ameshaandaa malipo yote kwa ajili ya kocha huyo.
“Mimi ndiye niliyekabidhiwa jukumu la kusimamia malipo ya Timbe na nimeshamkabidhi mhasibu, hivyo tunatarajia kumlipa madai yake ndani ya siku mbili,”alisema.
Bhinda alisema fedha atakazolipwa kocha huyo ni mishahara yake yote kwa miezi iliyobaki na malipo mengine kwa mujibu wa mkataba.
Hata hivyo, Bhinda hakuwa tayari kuweka wazi kuhusu malipo hayo kwa madai kuwa ni siri ya klabu na Timbe.
Yanga imeamua kukatisha mkataba na Timbe kwa madai ya timu kushuka kiwango na pia kutokuwa tayari kupokea maelekezo ya mabosi wake. Mkataba wa kocha huyo ilikuwa umalizike Mei mwakani.
Badala yake, klabu hiyo sasa imemrejesha kocha wake wa zamani, Kostadi Papic kutoka Serbia, ambaye alitimuliwa Februari mwaka huu.

No comments:

Post a Comment