KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, October 27, 2011

Watu wanapenda kuniita 'mtu wa totoz'-Van Vicker


LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu Van Vicker kwa sasa si mgeni tena katika fani hiyo nchini Nigeria. Ni mzaliwa wa Ghana, lakini amejipatia sifa kubwa kwa kucheza filamu za Kinigeria.
Mbali ya kuwa mwigizaji nyota, Van Vicker amejaliwa kuwa na sura nzuri na umbo lenye mvuto, kiasi kwamba mioyo ya wanawake wengi hufa kwake.
Akihojiwa na mtandao mmoja nchini Nigeria hivi karibuni, Van Vicker alisema licha ya mafanikio aliyofikia katika fani hiyo, changamoto kubwa kwake ni kukosekana kwa ushindani nchini Ghana.
Van Vicker alisema wapo wacheza filamu wengi nchini Ghana, lakini idadi yao haiwezi kulinganishwa na ile iliyopo Nigeria.
“Tunahitaji kuwa na waigizaji wengi zaidi, ndio sababu najisikia vibaya,”alisema mwigizaji huyo, anayepapatiwa na akinadada wengi kutokana na uzuri wa sura yake.
Van Vicker alisema alianza kucheza filamu za Kinigeria baada ya kushirikishwa katika filamu moja iliyochezwa kwa ushirikiano kati ya waigizaji wan chi hizo mbili.
Kwa mujibu wa mcheza filamu huyo, alijitosa katika fani hiyo miaka sita iliyopita baada ya mtayarishaji mmoja wa filamu nchini Ghana kuvutiwa na mwonekano wake. Awali, alikuwa mtangazaji wa radio na televisheni.
“Sidhani iwapo mwonekano wangu ndio ulioniwezesha nipate nafasi ya kucheza filamu. Walikuwa wakihitaji mtu makini na mwenye kujiamini. Binafsi ninajiamini na Mungu amenijalia kuwa na sura nziri,”alisema.
Van Vicker alisema si kweli kwamba kufanana kwake na Ramsey Noah ndiko kulikochangia kumfanya awe maarufu. Alisema yeye na Ramsey ni waigizaji wenye mwonekano na mambo tofauti.
Licha ya kupendwa na wanawake wengi, Van Vicker alisema anampenda na kumheshimu mke wake, ambaye walifunga ndoa miaka minane iliyopita.
Mcheza filamu huyo alisema, alifunga ndoa na mkewe wakati akiwa na umri wa miaka 26 na kuongeza kuwa, alifanya hivyo kwa sababu wakati ulikuwa umewadia na alimpata mwanamke anayependeka.
Van Vcker alikiri kuwa, Nigeria imepata mafanikio makubwa katika fani ya filamu, ikilinganishwa na Ghana, kwa sababu ilianza mapema zaidi. Alisema ana hakika tofauti hiyo itapungua hivi karibuni.
Alisema haelewi ni kwa nini watayarishaji wengi wa filamu nchini Nigeria, hupenda kumpa nafasi kwenye filamu za mapenzi. Alisema sababu hiyo ndiyo iliyomfanya aamue kuandaa filamu yake, atakayocheza nafasi tofauti.
Baadhi ya filamu za Ghana alizoshiriki kucheza ni pamoja na Divine love, Darkness for sorrow na Beyonce Mummy wakati zile za Kinigeria ni Woman’s Hour, Total Love, ‘One More Kiss na Opposite Attraction.

No comments:

Post a Comment