KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, October 27, 2011

'Sijivunii makalio yangu'



LAGOS, Nigeria
MWIGIZAJI filamu machachari wa Nigeria, Anita Joseph amesema si kweli kwamba, amekuwa akiyatumia makalio yake makubwa kama kishawishi cha kupata nafasi ya kucheza filamu nyingi.
“Mimi ni mwanamke mzuri na kila sehemu ya mwili wangu ina thamani kubwa. Kama nitapoteza mkono leo, hayo makalio yangu hayawezi kuwa na mvuto,”amesema Anita katika mahojiano na mtandao mmoja mjini hapa juzi.
Anita alisema pia kuwa, uamuzi wake wa kujitosa katika fani ya muziki haukulenga kupata mafanikio ya haraka.
Alisema biashara ya muziki sio sawa na sherehe ya kunywa chai na kuongeza kuwa, inachukua muda mrefu kwa mwanamuziki kupata mafanikio.
“Ninachokifanya ni kujitahidi kutoa kitu bora ili kuhakikisha, kila atakayetoa pesa na kutumia muda wake kununua albamu yangu, anafurahia kazi yangu,”alisema.
Anita, ambaye moja ya sifa zake ni kujazia kike, alisema kwa sasa anajiandaa kuibuka na singo zake mbili, zinazojulikana kwa majina ya ‘Yem something’ na ‘Money’.
Mwanadada huyo amekiri kuwa, katika siku za hivi karibuni amekuwa bize kutokana na kushiriki kucheza filamu zaidi ya saba kwa wakati mmoja.
Alizitaja baadhi ya filamu hizo kuwa ni Place scandal, Open and close, Under my bed, Million love, Festival of madness, Prince and Princess , The Kingdom is mine, I am the king naBest dancer.
Anita ameitaja filamu ya Titanic battle kuwa ndiyo iliyompa changamoto kubwa kwa vile alikaribia kupoteza maisha kutokana na nafasi aliyoicheza.
Alisema mara baada ya tukio hilo, alifikiria kujitoa kwenye fani hiyo, lakini alilazimika kufikiria upya uamuzi huo kabla ya kubadili mawazo.
Mcheza filamu huyo amesema, amekuwa akishiriki kucheza filamu zilizoandikwa vizuri kwa vile anakuwa na uhakika wa kutoa mchango wake kuzipendezesha.

No comments:

Post a Comment