KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, October 27, 2011

Platini ampiga dongo Beckham



PARIS, Ufaransa
RAIS wa Shirikisho la Soka la Ulaya (UEFA), Michel Platini ameitaka klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) kumsahau nahodha wa zamani wa England, David Beckham.
Nguli huyo wa zamani wa Ufaransa, alisema juzi kuwa, Beckham (36) hana kiwango bora kama zamani na amebaki jina, kauli ambayo huenda ikaibua mzozo kati yake na kiungo huyo wa Los Angeles Galaxy ya Marekani.
Kauli hiyo ya Platini imekuja baada ya kuwepo na taarifa kuwa, PSG inataka kumsajili winga huyo wakati wa usajili wa dirisha dogo Januari mwakani.
Platin alisema kitendo cha PSG kumsajili Beckham ni sawa na kupoteza muda au fedha.
"Beckham amekuja Paris kununua vitu, nampenda sana, lakini kwa sasa si mchezaji bora kama zamani," alisema Platini.
Alisema nguli huyo amekwenda Ufaransa kununua bidhaa na si kusajiliwa. Beckham, amepewa ofa ya kujiunga na klabu ya PSG kutoka kwa mkurugenzi wa ufundi, Leonardo aliyewahi kumfundisha AC Milan alipocheza kwa mkopo.
Mkataba wa mchezaji huyo unamalizika mwezi ujao na klabu kadhaa za Ulaya zimetuma maombi ya kumsajili. Klabu hizo ni Queens Park Rangers na Tottenham Hotspurs.

No comments:

Post a Comment