KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, October 20, 2011

Simba yambania Jerry Santo


UONGOZI wa klabu ya Simba umesema hauna mpango wa kumuuza kiungo wake, Jerry Santo kwa klabu nyingine.
Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema mjini Dar es Salaam juzi kuwa, Santo bado ni mchezaji halali wa klabu hiyo. Kamwaga alisema wameshafanya mazungumzo ya awali na Santo ili aweze kuongeza mkataba wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo.
Kwa mujibu wa Kamwaga, uamuzi wa kumuongezea mkataba Santo umefikiwa na benchi la ufundi la timu hiyo kutokana na kuridhika na uwezo wake.
“Jambo la msingi ni kwamba hatuna mpango wa kumwachia Santo akajiunge na klabu nyingine kwa sababu bado tunamuhitaji,”alisema.
Simba imeelezea msimamo wake huo baada ya baadhi ya vyombo vya habari kuripoti hivi karibuni kuwa, mchezaji huyo anatarajiwa kwenda kucheza soka ya kulipwa nje ya nchi.
Vyombo hivyo vya habari vilieleza kuwa, Santo amepanga kwenda nje baada ya mkataba wake na Simba kumalizika mwishoni mwa mwaka huu.

No comments:

Post a Comment