KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, October 20, 2011

GERRARD: Sikutegemea


LONDON, England
NAHODHA wa timu ya soka ya Liverpool ya England, Steven Gerrard, amesema hakutarajia kurejea kwenye kiwango bora baada ya kuwa nje ya uwanja kwa miezi sita.
Gerrard alirejea uwanjani kwa mara ya kwanza mwishoni mwa wiki iliyopita wakati Liverpool ilipomenyana na Manchester United katika ligi kuu ya England na kutoka sare ya bao 1-1.
Nahodha huyo wa Liverpool alifanyiwa upasuaji wa ngiri na kumfanya ashindwe kucheza soka kwa muda mrefu.
Gerrard alisema alipokuwa akiuguza majereha hayo, alidhani ungekuwa mwisho wake wa kucheza, soka lakini baada ya kucheza kwa ustadi dhidi ya United, anajiona ni mchezaji mpya.
"Nimepitia kipindi kigumu sana, miezi sita nje ya uwanja ni mingi na nilidhani nimekwisha. Lakini naendelea kurejea katika hali yangu ya kawaida siku hadi siku," alisema mchezaji huyo.
Gerrard (31) alidokeza kuwa, kabla ya kufanyiwa upasuaji, alikuwa akipigwa sindano za maumivu ili acheze baadhi ya mechi, hatua ambayo alidai haikuwa sahihi, lakini alilazimika kufanya hivyo ili kuokoa jahazi Liverpool.
Aliongeza kuwa, alilazimika kutumia muda mfupi kufanya mazoezi msimu uliopita kwa hofu ya kujitonesha.
“Miezi sita iliyopita ilikuwa kipindi kigumu kwangu katika maisha yangu kisoka,”alisema nguli huyo.
Mchezaji huyo ndiye injini ya Liverpool na amekuwa akitoa mchango mkubwa katika kikosi hicho.
Kocha Mkuu wa timu hiyo, Kenny 'King' Dalglish amesema Gerrard atakuwa nahodha wa muda mrefu.

No comments:

Post a Comment