KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, October 20, 2011

Van Persie aipa kiwewe Arsenal


LONDON, England
KLABU ya Arsenal ya England inakabiliwa na mtihani mgumu wa kumzuia nahodha wake, Robin va Persie baada Real Madrid ya Hispania kutenga pauni milioni 30 (sh. bilioni 69) kwa ajili ya kumsajili.
Kocha Mkuu wa Real Madrid, Jose Mourinho ametumia uamuzi wa Van Persie kuuza nyumba yake mjini London kumzengea wakati wa usajili wa dirisha dogo Januari mwakani.
Mholanzi huyo amebakiza miezi sita kabla ya mkataba wake na Arsenal kumalizika, ambapo atakuwa mchezaji huru na Mourinho amepanga kumng'oa kwa dau kubwa ili kujenga kikosi imara.
Mourinho, aliyeiongoza Real Madrid kuilaza Lyon mabao 4-0 katika ligi ya mabingwa wa Ulaya juzi, anataka kujenga safu imara ya ushambuliaji licha ya kuwa na Cristiano Ronaldo na Karim Benzema.
Hata hivyo, Mourinho atakuwa na kazi ngumu ya kumsajili Van Persie kutokana na ukweli kuwa ndio lulu ya kocha Arsene Wenger kwa ufungaji mabao.
Wenger alimpa unahodha Van Persie baada ya kuondoka Cesc Fabregas msimu uliopita, aliyetimkia Barcelona.
Wachezaji wengine walioihama klabu hiyo majira ya kiangazi ni Gael Clichy na Samir Nasri waliotua Manchester City.
Katika hatua nyingine, Wenger amesisitiza kuwa hana mpango wa kuondoka Arsenal kwa sasa.
Wenger ameelezea msimamo wake huo juzi, siku moja baada kuripotiwa kuwa, ameamua kuondoka klabu hiyo kabla ya mkataba wake kumalizika.
Kuna habari kuwa, tayari klabu ya PSG ya Ufaransa ilishaanza kujiandaa kumnyakua kocha huyo kwa kumfanya mkurugenzi wa michezo.
“Nimesaliwa na miaka mitatu kwenye mkataba wangu na Arsenal na siku zote nauheshimu mkataba wangu,”alisema kocha huyo.

No comments:

Post a Comment