KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, October 20, 2011

Mapacha wa Mariah Carey hadharani


NEW YORK, Marekani
MWANAMUZIKI nyota wa Marekani, Mariah Carey na mumewe Nick Cannon, wamewatoa hadharani watoto wao mapacha, Monroe na Moroccan.
Hii ni mara ya kwanza kwa Mariah na mumewe kuwaonyesha watoto hao hadharani, tangu walipozaliwa Aprili 30 mwaka huu.
Mariah (41) na Cannon walikwenda na watoto wao kwenye mahojiano maalumu yaliyofanyika katika kipindi na mtangazaji, Barbara Walters kuhusiana na ndoa yao.
Wakati wote wa mahojiano hayo, Monroe na Moroccan walionyesha uchangamfu.
Monroe, ambaye ni msichana, alibebwa na mama yake na Moroccan muda mwingi alikuwa kwa baba yake. Mariah alisema mapacha hao wamewapa majina ya utani ya 'Roc na Roe'.
"Mwili wangu ulikuwa mkubwa sana. Kuwatunza watoto wawili mapacha muda mrefu, si jambo dogo, lakini imewezekana. Kimsingi ilikuwa ni hatari," alisema Mariah.
Cannon alisema mtoto wake wa kike Monroe amefanana na mama yake Mariah.
"Watoto wetu ni wachangamfu, kila asubuhi wanapoamka, huonyesha sura za tabasamu, kama wana njaa utawabaini," alidokeza muigizaji huyo.

No comments:

Post a Comment