KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, October 27, 2011

TEVEZ ALIMWA FAINI BIL. 1/-


LONDON, England
KLABU ya Manchester City ya England imemtoza faini ya pauni 800,000 (sh. bilioni 1.8) mchezaji wake Carlos Tevez na ipo tayari kukatisha mkataba wake wa miaka mitatu.
Man City imempa adhabu hiyo Tevez kwa madai ya kugoma kucheza mchezo wa ligi ya mabingwa wa Ulaya dhidi ya Bayern Munich ya Ujerumani, uliopigwa mwezi uliopita kwenye Uwanja wa Allianz Arena.
Kufuatia adhabu hiyo, Tevez amesema atamshitaki Kocha wa Man City, Roberto Mancini kwa kumchafulia jina kwa kumtuhumu kugoma kucheza mchezo huo.
Kabla ya adhabu hiyo, Tevez anayelipwa mshahara wa pauni 198,000 (sh. milioni 455) kwa wiki, alifungiwa kwa wiki mbili.
Wakati huo huo, Mancini amesema Mwenyekiti wa klabu hiyo, Khaldoon al Mubarak amechukizwa na kitendo cha utovu wa nidhamu kilichoonyeshwa na Tevez kwa madai kimewavunjia heshima mashabiki na Manchester City.
Licha ya mshambuliaji huyo wa Argentina kutakiwa na klabu za Ulaya na Brazil, Man City imesema haitamuuza kwa bei rahisi.
Tayari klabu za Corinthians, Boca Juniors na Juventus zimesema zipo tayari kumsajili katika usajili wa dirisha dogo Januari mwakani.
Rais wa Corinthians, Andres Sanchez amesema wana uhakika wa kumsajili na mashabiki wanamsubiri kwa hamu. Man City imesema mchezaji huyo anauzwa kwa pauni milioni 40 (sh. bilioni 92).

No comments:

Post a Comment