KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, March 7, 2012

Namshukuru Mungu sina kashfa-Chioma




LAGOS, Nigeria
BAADA ya ukimya wa muda mrefu, mwigizaji nyota wa kike nchini Nigeria, Chioma Chukwuka amesema anamshukuru Mungu kwa kutoandamwa na kashfa tangu alipojitosa katika fani ya filamu.
Chioma ameueleza mtandao wa nigeriafilms wiki hii kuwa, bila ya Mwenyezi Mungu, asingeweza kupata mafanikio yoyote katika fani ya uigizaji filamu.
“Ni sala pekee kwa kila ninalotaka kulifanya ndizo zimenifanya nifike hapa nilipo,”alisema mwanadada huyo mwenye sura na umbo lenye mvuto.
“Lakini pia lazima niseme kwamba ni mapenzi ya Mungu. Kama siyo hivyo, kazi ngumu zinaweza kufanyika bila kutambulika,”aliongeza mwanadada huyo mwenye tabasamu la kukata na shoka.
Chioma amemshukuru Mungu kwa kumpa uwezo wa kufanyakazi kwa bidii na pia kumwezesha kupata mafanikio katika fani hiyo.
“Hakuna siri ya mafanikio haya kwa sababu kila unapomweka mbele Mungu katika kazi zako, lazima upate mafanikio katika jambo lolote, huwezi kukumbana na kikwazo,”alisisitiza.
Alipoulizwa ni kwa nini hajawahi kukumbwa na kashfa yoyote tofauti na waigizaji wengine wa kike wa Nollywood, Chioma alisema ni kwa sababu siku zote amekuwa akijichukulia kuwa mtu wa kawaida.
Chioma amesema kamwe katika maisha yake hapendi kujihusisha na mambo yasiyokuwa na maana na kwamba amekuwa akitumia muda wake mwingi kushughulikia masuala ya kifamilia.
“Kama usiponiona kwenye skrini ya sinema, basi ujue nipo na familia yangu nyumbani,”alisema.
Mwanadada huyo alisema siku zote binadamu anahitaji muongozo wa Mungu ili umsaidie kwenda katika njia iliyo sahihi katika kazi na maisha yake.

No comments:

Post a Comment