KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 1, 2012

EMEM: Sijavunja ndoa ya Monalisa


LAGOS, Nigeria
MTAYARISHAJI maarufu wa filamu katika Nollywood, Emem Isong amekanusha madai kuwa, amechangia kwa kiasi kikubwa kuvunjika kwa ndoa ya mcheza filamu nyota wa nchi hiyo, Monalisa Chinda.
Akihojiwa na mtandao wa nigeriafilms wiki hii, Emem alisema licha ya taarifa hizo kumsikitisha, pia zimemfadhaisha kwa sababu hazina ukweli wowote.
“Nilijisikia vibaya sana na kushangaa kwa nini walizusha maneno hayo?” Alisema Emem.
“Kwani mimi ni Mungu? Nawezaje kuvunja ndoa ya mtu mwingine? Ni jambo la kawaida kutokea katika maisha ya binadamu,”aliongeza mwanamama huyo.
Emem alisema Monalisa ni rafiki yake wa muda mrefu na walikuwa na kawaida ya kutembeleana mara kwa mara.
Kwa mujibu wa Emem, kila Monalisa alipokuwa na tatizo, alipenda kwenda kupumzisha akili nyumbani kwake na haoni iwapo kwa kufanya hivyo, alishiriki kuiparaganyisha ndoa yake.
Alisema hadi sasa haelewi ni kwa nini watu wamemzushia maneno hayo, lakini alisisitiza kuwa, Mungu ndiye anayeujua ukweli wa jambo hilo.
Emem amejitokeza kuwa mtayarishaji maarufu wa filamu nchini Nigeria na filamu zake nyingi zimejizolea umaarufu mkubwa. Emen ni mkali katika kuandika maelezo ya filamu na amekuwa akiifanyakazi hiyo kwa zaidi ya muongo mmoja sasa.

No comments:

Post a Comment