KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 1, 2012

Omotola akana kuwa mja mzito


LAGOS, Nigeria
BAADA ya ukimya wa muda mrefu, hatimaye mwigizaji machachari wa Nigeria, Omotola Jalade amekanusha madai kuwa ana uja uzito.
Omotola aliueleza mtandao wa nigeriafilms wiki hii kuwa, taarifa hizo ni za uzushi na hazina ukweli wowote.
Mwanamama huyo mwenye watoto wanne ameamua kueleza ukweli wa mambo baada ya baadhi ya vyombo vya habari kuripoti hivi karibuni kuwa, ni mja mzito.
Vyombo hivyo vya habari vilidai kuwa, Omotola amekuwa haonekani hadharani mara kwa mara kwa vile hataki ijulikane kwamba ana uja uzito.
“Hizi ni taarifa za kushangaza sana na sijui wamezipata wapi,”alisema mwanamama huyo mwenye sura na umbo lenye mvuto.
“Tulianza na tatizo la umeme na sasa linaishia kwenye tuhuma za uja uzito. Ndio tatizo la umaarufu,” aliongeza mama huyo, aliyecheza filamu zaidi ya 80.
Baadaye, mwanamama huyo aliandika kupitia mtandao wa tweeter:“Kile watu wanachokiandika, ndicho watu wanachokisoma.”
Omotola, ambaye pia ni mwanamuziki nyota nchini Nigeria, alitimiza umri wa miaka 34, ilipofika Februari 7 mwaka huu na amezaa watoto wanne na mumewe, ambaye ni rubani wa ndege, Matthew Ekeinde.
Mbali na kuwa mwigizaji na mwanamuziki, Omotola pia anamiliki taasisi, ambayo inajihusisha na kuwasaidia watoto yatima na wenye matatizo.

No comments:

Post a Comment