KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 1, 2012

D'Banj kwa mademu!


LAGOS, Nigeria
MWANAMUZIKI nyota wa Nigeria, Dapo Daniel Oyebanjo ameelezwa kuwa ndiye anayeongoza kwa kuwa na wapenzi wengi nchini humo.
Dapo, ambaye ni maarufu zaidi kwa jina la D’Banj anadaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wacheza filamu wengi wa Kinigeria.
Baadhi ya waigizaji wanaotajwa kumzimia mwanamuziki huyo ni pamoja na Genevieve Nnaji, ambaye amekuwa akikanusha madai hayo.
Genevieve alikaririwa hivi karibuni akidai kuwa, hana uhusiano wa kimapenzi na D’Banj na kwamba urafiki wao ni kama wa kaka na dada.
Mbali na Genevieve, mwanamuziki huyo pia alidaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mcheza filamu tajiri wa kike nchini humo, Ini Edo.
Waigizaji wengine wa kike, ambao wamewahi kuwa na uhusiano wa kike na D’Banj ni pamoja na Nadia Buari, Ruky Sanda, Mercy Johnson, Empress Njamah, Abiola Bashorun na mtangazaji wa channel O, Nonhle Thema.
Mzaliwa huyo wa Jimbo la Ogun pia amedaiwa kuwa na uhusiano na Amina Abubakar, binti wa makamu wa rais wa zamani wa Nigeria, Alhaji Atiku Abubakar na Jennifer Obayuwama, ambaye ni binti wa Polo Boss

No comments:

Post a Comment