KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, March 7, 2012

Kaburu: Tutaimudu ES Setif


UONGOZI wa klabu ya Simba umejigamba kuwa, hauna wasiwasi wa kupambana na ES Setif ya Algeria katika mechi ya raundi ya pili ya michuano ya Kombe la Shirikisho.
Makamu Mwenyekiti wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ alisema mjini Dar es Salaam juzi kuwa, wamepanga kujiandaa vyema kabla ya kumenyana na ES Setif.
Simba na ES Setif zinatarajiwa kuvaana Machi 25 mwaka huu katika mechi ya awali ya raundi ya pili itakayochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kabla ya kurudiana wiki mbili baadaye mjini Algiers.
Wekundu hao wa Msimbazi walifuzu kucheza raundi hiyo baada ya kuitoa Kiyovu ya Rwanda kwa jumla ya mabao 3-2.
“Taarifa tulizonazo ni kwamba wapinzani wetu, ES Setif ni wazuri, lakini nasi tutahakikisha tunajipanga vyema kukabiliana nayo,”alisema Kaburu.
Kaburu alisema kamati ya utendaji ya klabu hiyo imepanga kukutana mara baada ya mechi ya ligi kati ya Simba na Kagera Sugar, iliyotarajiwa kuchezwa jana kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Alisema katika kikao hicho, wajumbe watapeana majukumu kuhusu nini kifanyike na kisimamiwe na nani, ikiwa ni pamoja na kutafuta taarifa za wapinzani wao.
Makamu Mwenyekiti huyo wa Simba amewataka wanachama na mashabiki wa klabu hiyo kutoa ushirikiano wa kutosha kwa viongozi ili kufanikisha mipango hiyo.
Alisema lengo la Simba msimu huu ni kuhakikisha timu hiyo inafuzu kucheza ligi ya nane bora ya michuano hiyo kama ilivyokuwa mwaka 2003.

No comments:

Post a Comment