KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 1, 2012

MZEE YUSSUF AWAPIGA BAO THABITI NA ALLY J

Mwimbaji nyota wa muziki wa taarab nchini, Mzee Yussuf amewabwaga mahasimu wake, Thabiti Abdul na Ally J katika shindano la kumtafuta nani mkali wa kupiga kinanda katika muziki huo.

Shindano hilo liliendeshwa kwa takriban mwezi mmoja kupitia blogu hii ya liwazozito, ambapo wasomaji wake walitakiwa kupiga kura ili kumchagua nani mkali kati yao.

Mmiliki wa blogu hiyo, Rashid Zahor amesema shindano hilo lilianza mwishoni mwa Januari na kumalizika Februari 29 mwaka huu.

Jumla ya kura zilizopigwa kwa washiriki wote wanne wa shindano hilo, akiwemo Chid Boy ni 47.

Mzee ni mwimbaji na kiongozi wa kundi la Jahazi, Thabiti ni mmoja wa wakurugenzi wa kikundi cha Mashauzi Classic, Ally J ni rais wa kundi la Five Stars Modern Taarab wakati Chid Boy ni mpiga kinanda wa Jahazi.

Mzee aliongoza kwa kupata kura 23, ambazo ni sawa na asilimia 48 ya kura zilizopigwa.

Thabiti alishika nafasi ya pili kwa kupata kura 14, ambazo ni sawa na asilimia 29 ya kura zilizopigwa.

Ally J alishika nafasi ya tatu kwa kupata kura saba, ambazo ni sawa na asilimia 14 ya kura zilizopigwa wakati Chid Boy alishika mkia kwa kupata kura tatu, ambazo ni sawa na asilimia sita.

Nachukua fursa hii kuwashukuru wale wote walioshiriki kupiga kura kwa ajili ya kumchagua nani mkali wa kupiga kinanda. Blogu yenu hii itaendelea kuwaandalia mashindano ya wasanii mbalimbali kwa lengo la kubaini ubora wao kupitia kwenye kazi zao.

No comments:

Post a Comment