KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 1, 2012

Basena atumia mawakili kuibana Simba


KOCHA wa zamani wa Simba, Moses Basena ameamua kuweka mawakili wawili kwa ajili ya kudai haki zake kwa klabu hiyo baada ya kuvunja mkataba kati yao.
Akizungumza kwa njia ya simu kutoka Uganda juzi, Basena alisema amefikia uamuzi huo baada ya kugundua kuwa, uongozi wa Simba unakwepa kumlipa haki zake.
Basena alisema tayari ameshawasiliana na mawakili hao na kuongeza kuwa, wanaweza kufungua kesi ya madai dhidi ya Simba wakati wowote.
Uamuzi wa Simba kufungua kesi hiyo umekuja baada ya Simba kuvunja mkataba wake wa miaka miwili na kumwajiri kocha mpya, Milovan Cirkovic kutoka Serbia.
Awali, kocha huyo kutoka Uganda aliwasilisha malalamiko yake kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kabla ya kuyapeleka kwa Shirikisho la Soka la Dunia (FIFA).
Uongozi wa Simba ulikaririwa hivi karibuni ukidai kuwa, umemtaka kocha huyo awasilishe vyeti vyake kabla ya kumlipa madai yake.
Alipouilizwa jana kuhusu suala hilo, Ofisa Habari wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema hana taarifa yoyote juu ya jambo hilo.

No comments:

Post a Comment