KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 29, 2012

Ommy Dimples apewa shavu na DJ Cleo

BAADA ya kutamba na kibao chake cha Nainai, msanii machachari wa muziki wa kizazi kipya nchini, Ommy Dimpoz ameamua kurekodi wimbo mwingine mpya.
Akizungumza na Burudani mjini Dar es Salaam wiki hii, Dimpoz alisema amerekodi wimbo huo kwa kushirikiana na msanii DJ Cleo wa Afrika Kusini.
Dimpoz alisema walirekodi wimbo huo kwenye studio za B Hits za Dar es Salaam wakati DJ Cleo alipofanya ziara ya kimuziki nchini.
Alisema tayari msanii huyo wa Afrika Kusini ameshaondoka na demo yenye wimbo huo kwa ajili ya kwenda kumalizia kazi ya kuurekodi nchini kwao.
“Nashukuru na nimefurahi sana kwamba nimepata bahati ya kurekodi wimbo na mmoja wa wasanii nyota wa muziki wa hip hop barani Afrika,”alisema Dimpoz.
“Nilichokifanya ni kumpatia demo yenye wimbo huo ili akamalizie kwao kazi ya kuingiza sauti na kuchanganya mipigo ili kuiongezea ubora na akishairejesha, wimbo utakuwa umekamilika,”aliongeza msanii huyo.
Dimpoz alisema wimbo huo utajulikana kwa jina la Tonight na ameurekodi katika miondoko ya soul. Alisema anatarajia wimbo huo utakuwa mkali zaidi ya Nainai.
Alisema ameamua kurekodi na DJ Cleo kwa sababu anataka kuwa msanii wa kimataifa na kuongeza kuwa, lengo lake lingine ni kuuza kazi zake barani Ulaya na Marekani.
Mbali na kuwa mwanamuziki, DJ Cleo ni mtayarishaji wa muziki, akiwa anamiliki studio yake binafsi nchini Afrika. Kwa sasa, mwanamuziki huyo anatamba kwa kibao chake cha Facebook.

No comments:

Post a Comment