KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Friday, March 2, 2012

Mashujaa yaibomoa tena Twanga Pepeta



BENDI ya muziki wa dansi ya Mashujaa Musica imezidi kuibomoa bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ baada ya kumyakua mnenguaji wake mahiri,Lilian Tungaraza maarufu kama ‘Intanet’.
Meneja wa Mashujaa Band Maximilian Luhanga alisema kwamba wamweamua kuwachukua wanamuziki hao ili kuimarisha bendi yao katika idara hizo na tayari wameshasaini mkataba wa kuitumikia bendi hiyo kwa miaka miwili ambao onyesho la utambulisho linatarajiwa kufanyika jumatano ijayo katika ukumbi wa Nyumbani Lounge.
Hii ni mara ya pili kwa Mashujaa kuibomoa Twanga Pepeta ambapo mapema mwaka huu ilimyakua mmmoja ya waimbaji mahiri, Charlz Gabriel ‘Chaz Baba’. Kwa hisani ya http://mamapipiro.blogspot.com/

No comments:

Post a Comment