KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Wednesday, March 7, 2012

Jim Iyke kuzindua albamu ya muziki



LAGOS, Nigeria
MCHEZA filamu mwenye makeke nchini Nigeria, Jim Iyke amekamilisha mipango ya kuzindua albamu yake mpya.
Jim alisema hivi karibuni mjini hapa kuwa, anatarajia kuzindua albamu hiyo baadaye mwezi huu.
Kwa mujibu wa Jim, uzinduzi wa albamu hiyo umepangwa kufanyika Machi 25 mwaka huu kwenye ukumbi wa klabu ya Aphrodisiac mjini Accra, Ghana.
Jim anakuwa mcheza filamu wa tano wa Nigeria kujihusisha na muziki. Wacheza filamu wengine wanaojihusisha na fani hiyo ni Genevieve Nnaji, Omotola Jalade, Desmond Elliot, Ramsey Nouah na Stella Damasus.
Hivi karibuni, Jim alirekodi vibao viwili akiwashirikisha wanamuziki nyota wan chi hiyo, 2Face Idibia na Puffy T. Vibao hivyo ni Who am I na Born to do this.

No comments:

Post a Comment