KWA HABARI ZA MICHEZO NA BURUDANI WASILIANA NASI KWA NAMBA 0719-153800 AU 0788-455808 AU EMAIL rashidzahor67@gmail.com '

Thursday, March 1, 2012

BONANZA LA TASWA MACHI 24


BONANZA la waandishi wa habari linaloandaliwa na Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo nchini (TASWA), limepangwa kufanyika Machi 24 mwaka huu kwenye ufukwe wa Msasani, Dar es Salaam.
Mkurugenzi wa Uhusiano wa Jamii na Sheria wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Steve Kilindo aliwaambia waandishi wa habari mjini Dar es Salaam jana kuwa, kampuni yake imepanga kutumia sh. milioni 62.5 kudhamini bonanza hilo.
Kilindo alisema wamepanga kutumia kiasi hicho cha pesa ili kuhakikisha kuwa, bonanza hilo linafanyika kwa kiwango na ubora wa hali ya juu.
Alisema waandishi wa habari ni wadau wakubwa wa kampuni yake hivyo lengo lao kubwa ni kuona bonanza hilo linafana kwa vyakula, vinywaji, burudani na michezo mbalimbali.
Mwenyekiti wa TASWA, Juma Pinto aliishukuru TBL kwa kudhamini bonanza hilo kwa mwaka wa tano mfululizo na kuongeza kuwa, limekuwa likitoa fursa nzuri kwa wadau wa habari kukutana na kufahamiana.
Pinto alisema bonanza hilo linatarajiwa kuwakutanisha waandishi wa habari 1,500 kutoka vyombo mbalimbali vya habari nchini, ambao watashindano katika michezo ya soka, netiboli, kuvuta kamba, riadha na mbio za kwenye magunia.

No comments:

Post a Comment